Tuesday, December 18, 2012

jacob zuma afanikiwa kutetea kiti chake.... ashinda kwa kura nyingi.. dhidi ya makamu wake wa Rais Montlanthe...


Rais Jacob Zuma amechaguliwa kwa mara nyingine kuwa kiongozi wa chama tawala nchini humo cha African National Congress ANC.
Zuma alipata idadi kubwa ya kura zilizopigwa na wajumbe elfu nne wa chama hicho wakati wa mkutano wao uliofanyika Mangaung.
Tangu mwanza wa zoezi hilo, Rais Zuma, alitarajiwa kushinda na idadi kubwa ya kura dhidi ya mpinzani wake wa pekee ambaye pia ni naibu makamu wa rais Kgalema Motlanthe.
Bwana Motlanthe sasa amepoteza nafasi yake ya naibu kiongozi wa chama hicho na mahala pake pamechukuliwa na mfanyabiashara maarufu na mwanaharakati dhidi ya ubaguzi wa rangi Cyril Ramaphosa, ambaye sasa atakuwa makamu wa rais wa Afrika Kusini.

Ramaphosa makamu mpya wa rais


Mshindi wa nafasi hiyo ndiye atakayekuwa na nafasi ya kushinda uchaguzi wa mwaka 2014.
Chama cha ANC kimeshika hatamu nchini Africa Kusini tangu kumalizika kwa utawala wa ubaguzi wa rangi mwaka 1994.
Polisi nchini humo, hapo jana waliwatia mbaroni watu wanne baada ya taarifa kuzagaa kwamba walikuwa na mpango wa kulipuwa ukumbi unaotumiwa na wajumbe hao wa chama cha ANC.
Baada ya uchaguzi huo kucheleweshwa kwa masaa kadhaa, zoezi la kupiga kura lilianza saa sita usiku na kukamilika majira ya saa moja asubuhi kwa saa za Afrika Kusini.
Wajumbe hao walioonekana wamechoka huku wakijifunika mablanketi walionyesha vidole vyao vikiwa na alama ya wino.
Wajumbe hao wamekuwa wakipiga kura kwa ajili ya nafasi ya uongozi wa juu wa chama hicho.
Wafuasi wa rais Zuma, tayari wanaendelea kusheherekea, kufuatia ushindi huo mkubwa.
Rais Zuma analaumiwa kwa kushindwa kupunguza umaskini au kutatua tatizo la ufisadi ndani ya chama cha ANC na serikali, wakati mwezi wa nane mwaka huu watu walishangazwa na jinsi polisi walivyowapiga risasi na kuwauwa wachimba madini 34 ambao walikuwa wamegoma.

Chanzo: BBC Swahili

No comments:

Post a Comment