Saturday, December 29, 2012

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI SERIKALI YAZUIA KUINGIZWA MAFUTA YA DIESELI YALIYO CHINI YA KIWANGO NCHINI


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA NISHATI NA MADINI



Mwezi Novemba 2012, Kampuni ya Addax Energy SA ya Uswisi
ilishinda zabuni ya sita ya kuingiza mafuta kwa pamoja chini ya utaratibu
unaosimamiwa na Kampuni ya uagizaji mafuta kwa Pamoja (PICL).
Zabuni hiyo ilikuwa ni kwa ajili ya mafuta ya Mwezi Desemba 2012 na
mwanzoni wa Januari 2013.

Utaratibu wa uagizaji wa mafuta kwa pamoja huzingatia pamoja na
mambo mengine viwango vya ubora wa mafuta kama vinavyoelekezwa na
Shirika la Viwango nchini (TBS). Aidha, TBS hukagua ubora wa mafuta
hayo kabla hayajaingia nchini.

Pamoja na aina nyingine za mafuta, Addax Energy SA ilipaswa kuleta
mafuta ya dieseli yenye ujazo wa MT 100,000 sawa na takriban lita
100,000,000 katika zabuni ya sita. Meli ya AL BURAG iliyobeba mafuta
hayo ilitakiwa kufika hapa nchini na kupakua mafuta kati ya tarehe 17
mpaka 20 Desemba 2012. Hata hivyo, meli hiyo ilifika tarehe 24 Desemba
2012 ikiwa imechelewa kwa siku nne kwa mujibu wa ratiba. Mafuta hayo
yalipimwa na TBS tarehe 26 Desemba 2012 na kugundulika kuwa yako
chini ya viwango vinavyotakiwa kwa Tanzania. Aidha, tarehe hiyo hiyo,
Kampuni binafsi ya Intertek Testing Services iliyoajiriwa na PICL pamoja na
Addax Energy SA ilipima mafuta hayo na kujiridhisha kuwa yalikuwa chini

ya viwango vinavyotakiwa.

Kwa kuzingatia hali hiyo Serikali imechukua hatua zifuatazo:

1. meiagiza PICL pamoja
I
YARUDISHWE yalikotoka,

2. Imeiagiza EWURA ichukuwe hatua stahiki za KISHERIA dhidi
ya Kampuni ya Addax Energy SA,

3. PICL ichukuwe hatua zinazotakiwa dhidi ya Kampuni ya Addax
Energy SA kulingana na MKATABA, na

4. Imeziagiza PICL pamnoja na EWURA kuhakikisha kuwa hali hii
haijirudii tena hapa nchini.

Aidha, Wizara ya Nishati na Madini inapenda kuwahakikishia wananchi
kuwa kutopokelewa kwa mafuta hayo yaliyo chini ya viwango
HAKUTAATHIRI upatikanaji wa mafuta ya dieseli nchini kwa kuwa kwa
sasa kuna mafuta ya kutosha.

Katibu Mkuu
Dar es Salaam, Desemba 28, 2012

No comments:

Post a Comment