Tuesday, December 18, 2012

ANC kupata viongozi wapya afrika Kusini leo....

Makamu wa Rais wa Afrika Kusini Montlanthe ndie mpinzani mkubwa wa Rais Jacob Zuma katika uchaguzi wa ANC leo.


Njama ya kushambila mkutano wa wajumbe wakuu wa chama tawala nchini Afrika Kusini, cha African national Congress ANC, imetibuliwa.
Msemaji wa polisi nchini humo amethibitisha tukio hilo, na kusema kuwa washukiwa wanne wenye asili ya kizungu wenya itikadi za siasa kali wamekamatwa.
Rais Jacob Zuma, na maafisa wengine wakuu wa serikali na wa chama hicho wanaohudhuria mkutano huo unaoendelea Mangaung, wamepewa ulinzi mkali.
Viongozi wapya wa chama hicho wanatarajiwa kuchaguliwa na wajumbe hao.
Chama cha ANC, kimekuwa madarakani tangu kumalizika kwa utawala wa wazungu walio wachache mwaka wa 1994.
Msemaji wa polisi Phuti Setati, ameliambia shirika la habari la Reuters kuwa washukiwa wanne ambao walikuwa wakipanga jinsi ya kuuweka bomu katika eneo la mkutano huo, unaofanyika katika chuo kikuu cha Free State iliyoko katika eneo la Mangaung.

Zuma kukabiliana na naibu wake

Mwandishi wa BBC Milton Nkosi, ambaye yuko katika eneo hilo anasema, hali ya ulinzi imeimarisha nje na ndani ya ukumbi wa mkutano huo.
Ameongeza kusema kuwa maafisa wa polisi wanayakagua magari yote na watu wanaoingia katika ukumbi huo kwa kutumia vifaa maalum na pia mbwa wa kunusa.

Rais Jacob Zuma aliufungua mkutano huo siku ya Jumapili na anawania muhula wa pili kuwa kiongozi wa chama cha ANC.
Hata hivyo Bwana Zuma, anakabiliwa na upinzani kutoka kwa naibu wake Kgalema Motlanthe.
Mmoja wa wafanyabiashara tajiri zaidi nchini Afrika Kusini Cyril Ramaphosa, amemuunga mkono rais Zuma kwa kuwania kiti cha naibu kiongozi wa chama hicho.
Bwana Ramaphosa alikuwa miongoni mwa watu mashuhuri waliochangia pakubwa wakati wa mpito kutoka kwa utawala wa kizungu hadi kwa utawa wa Afrika walio wengi.
Katika hotuba yake ya ufunguzi, katika eneo hilo la Mangaung, ambako chama hicho kiliundwa karibu karne moja iliyopita, rais Zum,a alisema kuwa Afrika Kusini iko tayari kwa awamu ya pili, ambayo atahakikisha kuafikiwa na maendeleo ya kijamii na kiuchumu yatayaokuwa na manufaa kwa raia wa nchi hiyo.
Matokeo ya uchaguzi wa viongozi wakuu wa chama hicho yanatarajiwa baadaye wiki hii.

Kura za uchaguzi wa uongozi wa chama tawala cha Afrika Kusini African National Congress, ANC, zinaendelea kuhesabiwa.
Wajumbe elfu nne wa chama hicho wamepiga kura zao usiku wa kuamkia leo katika ukumbi wa mkutano wa ANC uliopo Mangaung.
Matokeo ya kura hiyo yanatarajiwa kutoka baadae leo hii.
Kiongozi wa chama hicho ambaye pia ni rais wa Africa Kusini, Jacob Zuma, anatarajiwa kupata ushindani mkali katika kinyang'anyiro cha nafasi hiyo kutoka kwa makamo wake Kgalema Motlanthe.

Matokeo kutangazwa leo

Mshindi wa nafasi hiyo ndiye atakayekuwa na nafasi ya kushinda uchaguzi wa mwaka 2014.
Chama cha ANC kimeshika hatamu nchini Africa Kusini tangu kumalizika kwa utawala wa ubaguzi wa rangi mwaka 1994.
Polisi nchini humo, hapo jana waliwatia mbaroni watu wanne baada ya taarifa kuzagaa kwamba walikuwa na mpango wa kulipuwa ukumbi unaotumiwa na wajumbe hao wa chama cha ANC.
Baada ya uchaguzi huo kucheleweshwa kwa masaa kadhaa, zoezi la kupiga kura lilianza saa sita usiku na kukamilika majira ya saa moja asubuhi kwa saa za Afrika Kusini.
Wajumbe hao walioonekana wamechoka huku wakijifunika mablanketi walionyesha vidole vyao vikiwa na alama ya wino.
Wajumbe hao wamekuwa wakipiga kura kwa ajili ya nafasi ya uongozi wa juu wa chama hicho.

Zuma kushindana na makamu wake wa rais Bw.Motlanthe

Bw. Motlanthe alimaliza minong'ono iliyokuwepo kwa kutangaza kuwania nafasi ya Zuma wiki iliyopita.
Siku ya Jumatatu, Bw. Motlanthe alisema hatasimama tena kuwania nafasi ya unaibu, msimamo ambao unaonekana kama njia ya kujiimarisha.
Kwa kuzingatia idadi ya kura anazopata kila mmoja, Zuma anatarajiwa kuibuka mshindi na kwa mujibu wa mwandishi wetu, huu ndio unaweza kuwa mwisho wa Bwana Motlanthe kisiasa.

Baadhi ya mashabiki wa rais Zuma, tayari washaanza kusheherekea, wakitarajiwa ushindi mkubwa.
Mpinzani mkubwa dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi na mfanyabiashara maarufu Cyril Ramaphosa naye anagombea nafasi ya naibu kiongozi wa chama, huku wachambuzi wa mambo wakisema hii inaonyesha jinsi rais Zuma anavyoungwa mkono.
Rais Zuma analaumiwa kwa kushindwa kupunguza umaskini au kutatua tatizo la ufisadi ndani ya chama cha ANC na serikali, wakati mwezi wa nane mwaka huu watu walishangazwa na jinsi polisi walivyowapiga risasi na kuwauwa wachimba madini 34 ambao walikuwa wamegoma.
Chanzo: BBC Swahili…




                                                      Wafuasi wa ANC.....

No comments:

Post a Comment