Wednesday, March 27, 2013

Kitabu cha 'Kifo ni haki yangu' cha Eric Shigongo chazinduliwa leo rasmi.

Mtunzi mashuhuri wa vitabu kutoka kampuni ya Mkuki na Nyota, Mzee Walter Bgoya, akikata utepe pamoja na mtunzi wa kitabu cha ‘Kifo ni Haki Yangu’, Eric James Shigongo (kulia) wakati wa uzinduzi wa kitabu hicho uliofanyika katika duka la vitabu la Tanzania Publishing House lililopo mtaa wa Samora jijini Dar es Salaam.

 Wapenzi wa vitabu vya Eric Shigongo wakipitia kitabu cha 'Kifo ni Haki yangu' wakati wa uzinduzi wake leo, pembeni mtunzi wa kitabu hicho akiwa anawatazama wasomaji wake walio pembeni namna wanavyofurahia matunda ya kazi yake.

Eric shigongo akiweka saini katika kitabu chake kipya 'Kifo ni Haki yangu' wakati wa uzinduzi leo.

Chanzo: Mjengwa website.

No comments:

Post a Comment