Tuesday, April 23, 2013

Ligi ya soka daraja la pili Mkoa wa Dar es Salaam yafikia patamu.


Na Mwandishi maalum.

LIGI Darajala la Pili Mkoa wa Dar es Salaam , hatua ya sita bora imezidi kushika kasi ambapo hadi sasa timu ya Red Coast inaongoza ligi hiyo kwa kujikusanyia pointi 7 baada ya kucheza mechi tatu.

Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam, Mohamed Mharizo, Red Coast imejikusanyia pointi hizo baada ya kuzifunga  Abajalo bao 1-0,  huku ikilazimishwa sare ya bila kufungana na Friends Rangers na jana Jumatatu iliichapa Sharif mabao 3-1, katika mechi iliyochezwa kwenye Uwanja wa Airwing.

Friends Rangers wanashika nafasi ya pili kwa kuwa na pointi 5, ilizozivuna kwa kutoka sare ya bila kufungana na Day Break katika mechi ya kwanza, kasha kulazimishwa  tena sare ya bila kufungana na  Red Coast na jana Jumatau iliifunga Boom FC bao 1-0 kwenye Uwanja wa Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa.

Abajao inashiaka nafasi ya tatu ikiwa na pointi 4, huku Sharif Star ikishika nafasi ya nne kwa kuwa na pointi 3, ikifuatiwa na Day Break yenye pointi 3 wakati Boom FC ikiburuza mkia kwa kuwa na pointi 1.

Kesho Jumatano ligi itaendelea kwa michezo mitatu, Abajalo vs Friends Rangers uwanja wa Kinesi, Red Coast vs Boom uwanja wa Makurumla na Sharif Stars vs Day Break uwanja wa Airwing. Ligi hiyo  inatazamiwa kumalizika Aprili 27 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment