Thursday, April 18, 2013

WARAKA WA WAZI KUTOKA MOSCOW KUENDA KWA WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUNGANO WA TANZANIA.



Mh Mizengo Kayanza Peter Pinda.
Mh Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania Mh Mizengo Kayanza Peter Pinda, naomba leo nizungumze na wewe kwa kutumia karamu na karatasi kuweza kufikisha kwako matatizo ya wanafunzi wa kitanzania wanaosoma nchini URUSI.

Mh Waziri Mkuu  mimi ni miongoni mwa wanafunzi ninaosoma nchi Urusi , kutokana na matatizo mbalimbali yanayotukabili wanafunzi wa kitanzania hapa URUSI , nimeona nitumie karamu na karatasi kuweza kufikisha matatizo haya kwako.

  1. MKOPO TUNAOPEWA HAUTUTOSHI KWASASA.
Mh waziri Mkuu, Mkopo tunaopewa kwa mwaka na serikali kupitia bodi ya mikopo ya elimu ya juu haitutoshelezi kulingana na gharama za maisha zilizopo kwa sasa huku Urusi.Tumeandika barua nyingi za kuomba kuongezewa angalau mkopo kwenda Bodi ya mikipo na wizara ya Elimu ya ufundi na mafunzo stadi na barua zetu kupitia Ubalozi wa Tanzania hapa Urusi toka mwaka 2009 mpaka 2012 lakini tumekuwa hatupatiwi majibu. Mheshimiwa kiukweli hali ya maisha imepanda sana hapa Urusi zaidi ilivyopanda huko nyumbani, kwani ada ya hostel mwaka 2008/9 ilikua dolar za kimarekani 660 kwasasa tunalipa dolar za kimarekani kati ya 1000 hadi 1200 kulingana na rate exchange ya siku utakayo lipia. Hili ni ongezeko la karibu asilimia 100% ukilinganisha na mwaka 2008. Mheshimiwa Waziri Mkuu kila kitu kipo juu huku mfano vyakula, usafiri , bima ya afya, stationaries(vitabu,karamu,madaftari na vifaa vingine ). Mheshimiwa Waziri Mkuu mkopo tunaopatiwa tunatakiwa tulipe hostel, chakula, usafiri, stationaries, facaulty requirement na mengineyo. Mheshimiwa Waziri Mkuu ukiwa kama mtendaji mkuu wa Serikali nakuomba uangalie upya mkopo tunaopatiwa wanafunzi wa Urusi na mwaka huu wa fedha wa 2013/14 angalau na sisi serikali iweze kutukumbuka kwa kutuongezea mkopo japo kidogo ili tuweze kukabiliana na ugumu wa maisha tunaopata huku.

Ili serikali iweze kujiridhisha naomba Mheshimiwa waziri Mkuu uweze kutuma ujumbe toka Wizara ya Elimu na Bodi ya mikopo waje huku Urusi waone hali halisi tunayokabiliana nayo sisi wanafunzi na wakijiridhisha na hali iliyopo huku serikali iweze kutuongezea mikopo mwaka huu wa fedha 2013/14.
Naimani Mheshimiwa utarifanyia kazi swala hili kwakua wewe ni mzazi na ni kiongozi usie bagua.

2.UCHELEWESHWAJI WA ULIPAJI WA ADA VYUONI.
Mheshimiwa Waziri Mkuu, serikali kupitia bodi ya mikopo imekua ikichelewa kulipa ada za wanafunzi katika vyuo mbalimbali hapa Urusi mpaka kupelekea usumbufu kwa wanafunzi kuzuiliwa kuingia madarasani hata kufanya mitihani, hili tatizo limekua likitokea kila mwaka na bodi ya mikopo imekua haionyeshi kama ipo tayari kulimaliza tatizo hili. Mheshimiwa Waziri Mkuu tatizo hili limekua likiitia serikali yetu aibu vyuoni kwani imefikia hatua vyuo husika havimsikilizi Balozi wetu Mh Jaka Mwambi anapokwenda vyuoni kuomba muda wa kulipa ada na wanafunzi wasiweze kusumbuliwa madarasani. Ninaamini kabisa kupitia ofisi yako hili tatizo la ucheleweshwaji wa malipo ya ada unaweza kulitatua na kulimaliza kabisa kwani ni kero sana kwetu wanafunzi hapa Urusi nadhani hata Kwa Maofisa wa Ubalozi Nchini Urusi.

3.UCHELEWESHWAJI WA MIKOPO KWA WANAFUNZI NA MAKATO YASIYO YA LAZIMA.
Mheshimiwa Waziri Mkuu, bodi ya mikopo kila mwaka imekua ikitucheleweshea mikopo yetu bila sababu za msingi, hauwezi amini mpaka leo hii kuna baadhi ya wanafunzi hajapatiwa mikopo yao na wakijaribu kuwasiliana na wahusika wa bodi hakuna majibu wanayopatiwa zaidi wanadanganywa na kutopokelewa simu zao, hawa watendaji wa bodi wanasahau kuwa sisi huku tupo ugenini hatuna baba, mama ,shangazi wala mjomba na wazazi wetu huku ni pesa tu maana bila pesa huku maisha ni magumu sana na watu tunapata stress  za ajabu sana. Nakuomba Mheshimiwa Waziri Mkuu uweze kuiagiza bodi ya mikopo iwalipe wanafunzi wote ambao bado hawajapatiwa mikopo yao ya mwaka wa masomo wa 2012/13 kwani ndugu zetu wanateseka bila sababu za msingi. Pia Mheshimiwa naomba bodi ya mikopo iwe inatupatia mikopo mapema kwani muhula wa masomo huku ni tofauti na nyumbani(Tanzania) kwani huku kila tarehe 1 ya mwezi septemba kila mwaka vyuo vyote hufunguliwa na wanafunzi wanaanza kusoma siku hiyohiyo ,sasa bodi kuchelewesha mikopo hata kwa wiki moja inatufanya tuanze semista tukiwa na msongo wa mawazo. Naimani tatizo hili utalishugulikia ili kutuondolea usumbufu usio wa lazima.

4.ULIPAJI WA BIMA YA AFYA KWA BAADHI YA WANAFUNZI.
Mheshimiwa waziri mkuu, kumekua na mtindo kwa bodi ya mkopo kutotupatia pesa ya bima ya afya kwa wanafunzi au kuwapatia baadhi pesa hizo na wengine tukikosa pesa hizo, hili ni tatizo kwani inapelekea mwanafunzi kuchukua pesa ileile ya matumizi ambayo tunalalamika haitoshi na kulipia bima ya afya, mfano mwaka wa masomo wa 2012/13 bodi iliwapatia baadhi ya wanafunzi pesa za bima ya afya na wengine kutopatiwa mpaka leo, inapelekea hisia mbaya miongoni mwetu juu ya watendaji wa bodi ya mikopo kuwa wanakula pesa zetu, maana haiwezekani nusu ya wanafunzi wapatiwe pesa ya bima ya afya wengine wasipatiwe. Naomba Mheshimiwa uliangalie hili tatizo na ulikomeshe maana linatufanya tuone watu wachache wanakula haki yetu. Pesa ya bima ya afya ni muhimu sana huku Urusi kwani bila bima ya afya huwezi kupatiwa matibabu hospitali yoyote ile.

5.OMBI LA KUPEWA PESA ZA KIJIKIMU KWA WANAFUNZI WANAOFANYA VIZURI NA KUPATA SCHOLARSHIP ZA SERIKALI YA URUSI.
Mheshimiwa Waziri Mkuu tunaomba serikali yako iangalie upya swala la kuwapatia mikopo ya pesa ya kujikimu tu kwa wale wanafunzi wanaokuwa wamefanya vizuri katika masomo yao mpaka kupelekea serikali ya URUSI kupitia vyuo husika kuwapatia scholarship ya Masters, kwani wanafunzi wengi huwa wanapata hizo scholarship lakini wanashindwa kusoma na kuamua kurudi nyumbani kutokana na kukosa pesa za kula, maana serikali ya Urusi hutoa ada na hostel tu. Hivyo naomba serikali kupitia wewe kama mtendaji mkuu wa serikali uliangalie hili swala kwani lina manufaa kwa Taifa na linaipunguzia serikali gharama ya kusomesha wataalamu nje ya nchi. Kwa kuwakopesha wanafunzi wanaofanya vizuri na kupatiwa scholarship na serikali ya urusi, itaamsha molari miongoni mwa wanafunzi tunaosoma huku ili tufanye vizuri na tuendelee kupata ujuzi mbalimbali huku kwa ajiri ya maendeleo ya taifa letu. Naimani Mheshimiwa Waziri Mkuu utalifanyia kazi swala hili kwani lina faida kwa Taifa.

6.TUNAOMBA NYONGEZA YA NAULI KWA WANAFUNZI WANAHITIMU MASOMO YAO URUSI.
Mheshimiwa Waziri Mkuu, karibu kila mwaka wanafunzi wa kitanzania wanahitimu masomo yao katika vyuo mbalimbali Nchini Urusi na inatakiwa warudi nyumbani kujenga na kuitumikia nchi yetu kwa kurudisha fadhira kwa serikali na watanzania kwa ujumla, Hivyo naomba serikali kupitia bodi ya mikopo kuangalia upya kiwango cha pesa ya nauli na mizigo inayotolewa kwa mwanafunzi anapohitimu kwani ni kidogo ukilinganisha na vitu alivyonavyo mwanafunzi aliyekaa karibu miaka sita (6) huku Urusi. Pia kuna wakati wanafunzi wanalazimika kuacha baadhi ya vitu vyao kwa kushindwa kusafirisha kutokana na ukata unaowakabili. Kwakua naamini serikali yako ni sikivu hivyo swala hili utalifanyia kazi mapema.

Mheshimiwa Waziri Mkuu naimani waraka huu utakufikia popote pale ulipo, Pia nichukue fursa hi kukutakia majukumu mema ya kitaifa uliyonayo hasa katika kipindi hiki kigumu cha Bunge la bajeti ya 2013/2014.
Wako katika ujenzi wa Taifa
Mwanafunzi wa kitanzania nchini Urusi.
Moscow ,2013.


No comments:

Post a Comment