Monday, August 13, 2012

Kamera ja jembe mtaani.... jana.

 Ajali bado inatafuna watu njia ya Dar es Salaam kwenda Tanga, hii haijadhuru mtu ila imeharibiwa na Scania

 Nilikuwa maeneo ya Chalinze mzee katika mizani, nikakuta hawa vijana wa kimasai wakisoma gazeti..

                           Huyu Raia wa kigeni sijui amepatwa na masaibu gani, Cghalinze hii.

 Huyu bwana alievalia sarun, ndie atakaekuwa msaidizi wa Jembe kutoka Tanga. Anaitwa Miraji Wandy.

 Hakika ukitaka Baiskeli nenda Tanga, hii ni Tanga Jana mchana, nilikutana na Kaka yangu huyu. Mimi nae ni watoto wa Shangazi kwa Mjomba. Anaitwa Humud Rashid Micheni. Ni mtoto wa Shangazi...

Tazama hizo picha mbili za Wamasai,moja nimeipiga mimi maeneo ya Shekilango, wamasai wakimsuka dada, Ya chini sijaipiga mimi nimeitoa Mjengwa blog, inaonyesha wamasai wakichoma nyama. Unaweza kuzitafsiri?

No comments:

Post a Comment