Wednesday, April 10, 2013

Ngamia wa zawadi kwa Rais wa Ufaransa kutoka Rais wa Mali, achinjwa.


Afisa mmoja mkuu nchini Mali anasema kuwa Mali inatarajiwa kumpelekea rais wa Ufaransa Ngamia mwingine baada ya yule wa kwanza waliokuwa wamempa kama zawadi kuchinjwa.
Rais Francois Hollande alimwacha Ngamia huyo na familia moja kumchungia baada ya kukabidhiwa na wenyeji kama zawadi mwezi Februari.
Wanajeshi wa Ufaransa walitumwa Mali mwezi Januari ili kuweza kutwa eneo la Kaskazini kutoka mikononi mwa wapiganaji wa kiisilamu
Alipompokea mnyama huyo, Bwana Hollande alisema kwa mzaha kuwa atamtumia kwa safari zake za jangwani.
Maafisa wa Ufaransa walikuwa wanapanga kumsafirisha mnyama huyo hadi Ufaransa na kumweka kwenye hifadhi ya wanyama lakini kwa sababu ya ugumu wa mpangilio wa safari hiyo, wakaamua kuikabidhi familia moja jukumu la kumchunga mnyama huyo.
Waziri wa ulinzi, wa Ufaransa alimfahamisha rais kuhusu kuchinjwa kwa Ngamia huyo.
Afisaa wa Mali alisema punde waliposikia kuhusu habari hiyo waliweza kumpa rais Ngamia mwingine ambaye walisema alikuwa na afya nzuri zaidi kuliko yule wa kwanza aliyekuwa amepewa.
Ngamia huyo mpya atapelekwa Paris. “Tumeaibika sana kwa kile kilichotokea. Ilikuwa zawadi na haikupaswa kufanywa hivyo,” Ilisema ofisi ya Rais wa Ufaransa.
Ufaransa ina wanajeshi 4,000 nchini Mali wakisaidiwa na Maelfu ya wanajeshi wa Mlai , Chad na kutoka nchi zingine za Afrika.
Chanzo: BBC Swahili.

No comments:

Post a Comment