Friday, April 5, 2013

Waziri Samia Suluhu atembelea Taasisi ya sayansi ya Bahari Zanzibar...

 Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Raisi Muungano Samia Suluhu Hassan akipata Maelezo  kwa Mhadhiri Mwandamizi wa Taasisi ya Sayansi ya Bahari Dkt Narriman Jiddawi juu ya Utunzaji wa Samaki Aquarium.


Waziri Samia Suluhu Hassan akipata Maelezo juu ya Ujenzi wa Kituo cha tasisi ya Sayansi za  Bahari kilichopo Chukwani Unguja  kwa Kaimu Mkurugenzi Dkt Christophet Muhando wakati waziri  alipofanya Ziara ya Kutembelea Tasisi za Jamhuri za Muungano wa Tanzania zilizopo Unguja   
 Mhadhiri Mwandamizi wa Tasisi ya Sayansi ya Bahari ya Chua Kikuu cha Dar es Salaam Dkt NarrimanJiddawi akimuonyesha Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano Samia Suluhu Hassan aina ya Kasa katika chumba cha Kutunzia samaki[AQUARIUM}wakati wa Ziara ya Kutembelea Tasisi za jamhuri ya Muungano wa Tanzania zilizopo Unguja .
 
Kaimu Mkurugemzi waTaasisi ya Sayansi ya Bahari ya chuo kikuu cha Dar es Salaam Dkt Christopher Muhando akimtembeza Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan kwenye Jengo la Taasisi ya Sayansi ya Bahari huko Chukwani Mjini Unguja wakati wa Ziara yakutembelea taasisi za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania[PIcha na Ali Meja]  


Na Ali Issa Maelezo, Zanzíbar.
ZAIDI ya shilingi bilioni 14 zinahitajika ili kukamilisha ujenzi wa chuo cha Taasisi ya  Sayansi za Bahari kilichopo Buyu Wilaya ya Magharibi nje kidogo ya mji wa Zanzibar.

Hayo yamesemwa leo huko Forodhani mjini Zanzibar na Muhadhiri Dkt. Ntahondi Nyandwi wakati alipokuwa akisoma ripoti ya chuo hicho na rasilimali zake mbele ya Waziri anayeshughulikia masuala ya Muungano Samia Suluhu Hassan aliyekuwa katika mfululizo wa ziara yake kuzitembelea Taasisi za muungano, Zanzibar.

Amesema fedha hizo zitahitajika ili kukamilisha ujenzi wa  jengo lote na miundombinu  ikiwemo vifaa vya maabara, sehemu za wanafunzi wa shahada za uzamili,  uzamivu, kumbi za mikutano, ofisi za programu za kimataifa, ofisi za wageni wa kimataifa na mengineyo.

Dk. Nyandwi amesema kupatikana kwa fedha  hizo kutakamilisha mahitaji hayo na mengine ambapo kwa sasa ujenzi huo umefikia  hatua nzuri  na wameshatumia zaidi ya bilioni nne  kwa kujenga miundo mbinu mbalimbali ikiwemo  ofisi za viongozi na madarasa.

“Kwa vile pesa za kumlipa mkandarasi hazikupatikana kwa wakati na hakukuwa na uhakika kuzipata, ujenzi ulisimama Agosti 2008 na mkandarasi aliondoka lakini kwa sasa ujenzi unaendeleo taratibu”alisema Nyandwi .

Aidha alifahamisha kuwa ujenzi huo unaendelea kidogo kidogo  kadri fedha zinavyo patikana baada ya kumuomba mkanda rasi awapunguzie gharama na kuweza kumaliza mipango ya awamu ya kwanza na ya pili.  

Nae Waziri wa  Nchi Afisi ya Makamu wa Rais,  Muungano  Samia Suluhu Hassan  amesema kuwa atamuagiza Mkuu wake wa kazi kuja Zanzíbar  kujionea na yeye   Jengo hilo hatua ilio fikiwa.

Aidha alisema kua ujenzi huo utaendelea kidogokidogo mpaka utapomalizika.

Maendeleo ya ujenzi wa Taasisi ya sayansi Baharini ni moja ya Taasisi za Chuo  Kikuu cha Dar-es Salaam kampasi  ya Mwalimu Nyerere ambapo umuhimu wa Taasisi hiyo ulianza kujitokeza Mwaka 1978 chini ya sheria Na. 12 ya 1970 ya chuo kikuu cha Dar-slamu kwa tamko la Serikali Na. 34 lililo pitishwa tarehe 16 march 1979.

Chuo hicho kumalizika kwake kufanya kazi za kutafiti nyanja zote za Sayansi za Baharini, kutoa mafunzo ya uzamivu, uzamili katika sayansi ya Bahari ,kutoa ushauri wa kitalamu ,kutoa mafunzo ya Shahada ya kwaza  kwa kulingsana na mahitaji ya  Taifa la Tanzania   kama sehemu ya Taluma kwa vitendo.

IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR 5/4/2013

No comments:

Post a Comment