Saturday, April 13, 2013

Rais Kikwete azindua rasmi barabara ya Horohoro inayounganisha Kenya na Tanzania kupitia Tanga - Mombasa.




Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akifungua rasmi  barabara ya Tanga – Horohoro leo, ambayo imejengwa kwa kiwango cha lami ikiwa na urefu wa kilomita 65.14 akisaidiana na Bw. Daniel Wolde Yohannes, Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Changamoto za Milenia wa Marekani (MCC), Balozi wa Marekani nchini Mhe Alfonso Lenhardt, Barabara hii  ya Tanga – Horohoro ni sehemu ya barabara inayoiunganisha Tanzania na nchi jirani ya Kenya kupitia mkoa wa Tanga.  Mradi huu umepata msaada wa Serikali ya Marekani kupitia Mfuko wa Changamoto za Milenia (Millennium Challenge Corporation – MCC). Kukamilika kwa barabara hii ni utekelezaji wa azma ya Serikali ya Awamu ya Nne ya kuboresha miundombinu muhimu ya usafiri wa barabara.  Aidha, kukamilika kwa barabara hii kutapanua fursa za kibiashara kati ya Tanzania na Kenya na hivyo kutumia vizuri zaidi fursa za Soko la Pamoja la Jumuiya ya Afrika Mashariki.


Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akipanda mti kama kumbukumbu yaq ufunguzi rasmi  barabara ya Tanga – Horohoro ambayo imejengwa kwa kiwango cha lami ikiwa na urefu wa kilomita 65.14. Kuhsorto kwake ni Bw. Daniel Wolde Yohannes, Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Changamoto za Milenia wa Marekani (MCC), na kulia kwake ni  Balozi wa Marekani nchini Mhe Alfonso Lenhardt.



Msafara wa Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete ukipita juu ya sehemu ya barabara ya Tanga – Horohoro.
Picha na IKULU. 

No comments:

Post a Comment