Monday, April 1, 2013

William Ruto aitembelea Tanzania kwa mara ya kwanza akiwa makamu wa Rais Mteule.

 JK akimuongoza kuelekea kwenye chakula cha mchana  Naibu Rais mteule wa Kenya Mhe William Kipchirchir Samoei Arap Ruto na mkewe Rachel Chebet katika hoteli ya kitalii ye Seronera katika mbuga ya wanyama ya Serengeti mkoani Mara. Mhe Ruto alikuwa nchini kwa mapumziko ya Pasaka.
 William Ruto akifurahia jambo na mwenyeji wake walipokuwa kwenye mazungumzo baada ya chakula kwenye mbuga ya wanyama ya Seronera Mkoani Manyara.

Familia ya William Ruto ikiwa katika picha ya pamoja na Rais Jakaya Kikwete mara baada ya kukamilisha ziara yao nchini Tanzania.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Mrisho Kikwete  amekutana na Naibu Rais mteule wa Kenya Mhe William Ruto ambaye alikuwa nchini kwa mapumziko ya Pasaka.

Akiongea na mgeni wake katika hoteli ya Seronera iliyoko katika mbuga ya wanyama ya Serengeti mkoani Mara, Rais Kikwete amempongeza Mhe Ruto na Rais mteule wa Kenya Mhe. Uhuru Kenyatta, kwa ushindi wao kwenye uchaguzi mkuu nchini Kenya.

Kikwete, pia alimuelezea Mhe Rutto furaha yake pamoja na kuridhishwa na namna uchaguzi ulivyofanyika kwa amani katika nchi hiyo.

Alizungumzia matumaini yake ya kuwa urafiki uliopo kati ya Tanzania na Kenya utadumishwa pamoja na kusukuma mbele gurudumu la maendeleo ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Mhe Rutto, ambaye aliwasili mkoani Mara wiki iliyopita akiwa na mkewe na watoto, ameondoka jana jumatatu baada ya chakula cha mchana alichoandaliwa na mwenyeji wake.

CHANZO: IKULU

No comments:

Post a Comment